MALENGO MAKUU YA IVST
Malengo makuu ya Itifaki ya Vijana kwa Mikutano na Sherehe Tanzania (IVST) ni kama ifuatavyo:
Kukuza na kuimarisha uelewa wa itifaki, maadili na nidhamu kwa vijana katika mikutano na sherehe mbalimbali nchini Tanzania.
Kutoa mafunzo ya kitaalamu kuhusu itifaki ya mikutano, sherehe na matukio ya kijamii na kitaifa.
Kuandaa na kuendeleza vijana kuwa Maafisa wa Itifaki (Protocol Officers) wenye ujuzi na maadili.
Kukuza uongozi bora, mawasiliano yenye heshima na uwajibikaji miongoni mwa vijana.
Kushirikiana na Serikali, taasisi za umma na binafsi, pamoja na jumuiya nyingine katika masuala ya itifaki na maendeleo ya vijana.
Kukuza uzalendo, heshima ya taifa na utamaduni wa Kitanzania kupitia utekelezaji wa itifaki sahihi.
DHIMA (MOTTO / KAULIMBIU)
“Maadili, Nidhamu na Heshima katika Kila Tukio.”


No comments: